IQNA

Chuki dhidi ya Uislamu

Rais wa Pakistan ahimiza hatua za kuzuia kuvunjiwa heshima Qur'ani Tukufu

15:16 - July 01, 2023
Habari ID: 3477222
Rais wa Pakistan Arif Alvi amelaani vikali kuvunjiwa heshima Qur'ani Tukufu nchini Uswidi (Sweden), huku akitaka kuchukuliwa hatua za kukomesha vitendo hivyo vya kufuru.

Katika ujumbe wake wa Twitter, alisema tukio hilo la uchungu limeumiza sana hisia za mabilioni ya Waislamu. Rais wa Pakistani alisema kila taifa lazima lichukue hatua za kuzuia vitendo hivyo vya chuki dhidi ya Uislamu.

Aliitaka jumuiya ya kimataifa kufanya kazi kwa ajili ya kukuza maelewano kati ya dini na mazungumzo ili kujenga kuvumiliana kwa imani na maadili ya kidini ya kila mmoja.

Alvi alisisitiza kuwa ubinadamu lazima uondokane na vitendo vya chuki zisizo na maana kuelekea kuunganisha ulimwengu kwa amani.

Mataifa mengi ya Waislamu kama Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Iraq, Saudi Arabia, Kuwait, Pakistan, Jordan na Uturuki yametoa taarifa za kulaani kitendo hicho cha kuvunjiwa heshima Qurani Tukufu nchini Uswidi siku ya Jumatano wakati wa kuanza siku kuu ya Idul Adha.

Habari zinazohusiana
Kishikizo: uswidi qurani tukufu
captcha