Idara ya Usimamizi wa Misikiti Miwili Mitakatifu ya Makka na Madina imesema maeneo hayo ni maalumu kwa walemavu hasa viziwi na walemavu wa macho.
Idara hiyo imesema watu wenye mafunzo maalumu wamewekwa katika maeneo hayo kuwasaidia wanaofika katika eneo hilo la ibada.
Kati ya huduma zinazotolewa hapo ni kufasiri kwa lugha ya ishara na kutoa mafunzo ya qiraa na tafsiri ya Qur’ani Tukufu.
Katika kipindi hiki cha janga la Corona maeneo hayo yatakuwa yakisafishwa na dawa maalumu za kuua virusi.