Hija ya mwaka huu ni ya aina yake kwani ni Waislamu takribani 1,000 tu watakaotekelza Ibada ya Hija kufuatia uamuzi wa utawala wa Saudia kupunguza idadi ya mahujaji ili kuzuia kuenea ugonjwa wa corona. Kwa kawaida kila mwaka Waislamu takribani milioni mbili na nusu kutoka kila kona ya dunia hutekeleza ibada ya Hija lakini mwaka hii ni watu 1000 tu ambao ni raia 300 wa Saudia na raia 700 wa kigeni wanaoishi Saudia.