IQNA

Mashindano ya Kitaifa ya Qur'ani yaanza Nigeria

17:22 - February 04, 2017
Habari ID: 3470833
IQNA-Mashindano ya 31 ya Kitaifa ya Qur'ani nchini Nigeria yameanza Ijumaa katika mji wa Ilorin jimboni Kwara magharibi mwa nchi hiyo ya Afrika Magharibi.

Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, mashindano hayo yameandaliwa na Kituo cha Masomo ya Kiislamu, Chuo Kikuu cha Usmanu Danfodiyo, jimboni Sokoto kwa ushirikiano wa Kamati ya Musabaqah ya Jimbo la Kwara.

Mashindano hayo yalianza Ijumaa 4 Februari na yanatazmaiwa kuendelea hadi Jumamosi, 11 Februari katika jimbo hilo.

Mwenyekiti wa kamati andalizi ya mashindano hayo, Jaji (Mstaafu) Idris Haroon amesema yanatazamiwa kuwa na washiriki kutoka majimbo 30 ya Nigeria na yanafanyika katika Ukumbi wa Al-Hikmah.

Jaji Haroon, ambaye aliwahi kuwa Kadhi Mkuu wa Mahakama ya Kiisalmu ya Rufaa ya Jimbo la Kwara, amesema washindi watatunukiwa zawadi katika sherehe zitakazofanyika katika Uwanja wa Metropolitan.

Kwa kawaida washindo wa mashindano hayo huteuliwa kuwakilisha Nigeria katika mashindano ya kimataifa ya Qur'ani maeneo mbali mbali duniani.

3570130
captcha