IQNA

Waislamu Marekani wapinga chuki dhidi ya Uislamu

22:57 - May 29, 2015
Habari ID: 3308862
Wajumbe wa Baraza la Uhusiano wa Kiislamu Marekani wameamua kuitisha mkutano na waandishi wa habari katika jimbo la Arizona ili kupambana na vitendo vya kueneza chuki dhidi ya dini hiyo tukufu ya Mwenyezi Mungu.

Tawi la baraza hilo katika jimbo la Arizona liliitisha mkutano na waandishi wa habari jana Ijumaa ili kupinga kitendo cha maadui wa Uislamu cha kukusanyika mbele ya msikiti wa Phoenix wa jimbo hilo.
Mkutano huo na waandishi wa habari umeitishwa na Waislamu hao ili kujibu kundi la wapanda pikipiki wenye silaha waliokusanyika mbele ya msikiti huo.
Jon Ritzheimer mwanajeshi wa zamani wa Marekani mwenye chuki kubwa dhidi ya Uislamu na ambaye ameandaa maandamano hayo ya kupinga Uislamu aliiambia televisheni ya CNN siku ya Alkhamisi kwamba wamejiandaa kutangaza waziwazi upinzani wao dhidi ya Uislamu.
Waislamu wa jimbo la Arizona wamewataka maafisa usalama wa Marekani walinde usalama wao hususan kutoka na Waislamu hao kupokea barua za vitisho zinazotishia maisha yao.

3308765

Kishikizo: marekani waislamu
captcha