Katibu Mkuu wa OIC Iyad Ameen Madani ametoa taarifa na kusema utawala wa Israel unapaswa kubebeshwa lawama kuhusu kuendelea hujuma dhidi ya Msikiti. Amesema vitendo vya Israel vitapelekea kuibuka vita vya kidini, misimamo mikali na ukosefu wa uthabiti katika eneo.
Utawala wa Kizayuni wa Israel unaendelea kuwawekea vizingiti Wapalestina wanaoenda kuswali katika msikiti wa al Aqsa. Uchunguzi umebaini kuwa asilimia 90 ya Wapalestina wanaamini kuwa Israel inatekeleza njama za kubomoa Msikiti wa Al Aqsa na mahala pake kujenga hekalu la Kiyahudi.../mh