Shirika hilo la kuuza nguo limekubali kumlipa Bi. Elauf dola za Kimarekani 25,000 baada ya kupatikana na hatia ya kumyima kazi kwa ajili ya vazi lake la Hijabu.
Mwezi uliopita Mahakama ya Rufaa Marekani ilipiga kura 8-1 na kuamua kuwa shirika la Abercrombie & Fitch lilikiuka haki za kidini ya Elauf kwa kukataa kumuajiri mwaka 2008 kama mfanaykazi katika duka la nguzo za watoto la Abercrombie Kids huko Tulsa, Oklahoma.
Shirika hilo mbali na kumlipa fidia Elauf limetakiwa pia kulipa gharama za mahakama zilizokadiriwa kuwa $ 18,983.
Kubagua mfanyakakazi kwa msingi wa kidini ni kinyume cha sheria za kifederali nchini Marekani isipokuwa pale itakapohisika kutakuwa na usumbufu mkubwa kwa mfanyakazi.
Pamoja na kuwa Elauf alipata pointi nyingi katika mahojiano lakini alinyimwa kwazi kwa ajili tu alikuwa amevaa mtandio.../mh