TEHRAN (IQNA)- Siku ya kwanza ya tamthilia ya kimataifa Taaziya imefanyika mjini Tehran katika medani ya Imam Hussein AS huku kukiwa na makundi ya wanatamthilia kutoka Nigeria na mji wa Isfahan, kati mwa Iran.
Taaziya ni tamthilia ijulikanyao kama Taziye inayosimulia kisa ya kuuawa Shahidi Imam Hussein AS na wafuasi wake katika jangwa la Karbala miaka 1382 tarehe 10 Muharram kulingana na kalenda ya Hijria Qamaria.