Mashindano hayo yalifanyika Jumatano ambapo washindi walitunikiwa zawadi punde baada ya mashindano kumalizika
Mashindano hayo ya siku moja yalifanyika katika Msikiti wa Fateh unaofungamana na Jumuiya ya Vituo vya Kiislamu ya Denmark.
Mkuu wa Jumuiya hiyo, Ilyas Kokcu akihutubu katika mashindano hayo alisisitiza kuwa kushinda au kushika nafasi ya kwanza si lengo la mashindano bali nia ni kuimarisha ufahamu wa Qur'ani Tukufu.
Aidha alitoa wito kwa wazazi Waislamu wawafunzo watoto wao msingi wa Qur'ani wa kuwa na maadili mema si kwajili ya faida za kidunia tu bali pia kwa ajili ya kesho Akhera.
Waislamu wanakadiriwa kuwa asilimia tano ya watu wote milioni sita nchini Denmark.